Kiongozi wa kundi la Mtanashati Entertainment Ostaz Juma na Musoma amejikuta katika wakati mgumu baada ya mashabiki kutoa mitazamo yao baada ya kupost picha katika mtandao wake wa kijamii wa inayomuonesha msanii Pnc akimpigia magoti akiwa ameambatanisha na maelezo yanayoonesha kile kilichodaiwa kuwa ni kejeli.
Soma alichokiandika Ostaz hapo chini
: “hahaha jamani mziki ni kazi pnc arudi kuomba msamaha ili aendelee kufanya kazi mtanashati.”

Status ya pili: “jamani mziki ni mgumu sana, pnc karudi kwa kuomba msamaha kwa boss wake Ostaz juma.”

Hali hiyo imetafsiria kama ni kitendo cha unyanyasaji dhidi ya msanii wake huyo waliyeingia naye katika tofauti.

Tazama baadhi ya maoni ya mashabiki hapo chini

Rashid Ibrahim Huo unyanyasaji hata kama ana pesa hakustahili kumfanyia hivyo jamani!

Gilbert Kyando Kuweka picha kama hiyo mtandaoni sio poa design kama kumchoresha jamaa lakin kuomba msamaha fresh maana jifanye mjinga siku ipite coz bora uwe mjinga kwa muda mfupi

Novia Maduka sio vizur namna hii kwan angesema tu kuwa kaomba msamaha ingemuuwa? Wanadam ndivyo tulivyo tunahesabu sana makosa....je ni nani angesimama mbele za Mungu kama angetuhesabia na sisi? HAKUNA!! Hata hivyo ukiinuliwa na mwanadam kumbuka ye ndo atakushusha chini tujifunze kumtegemea Mungu na kutumia akili alizotupa.
Je wewe mtazamo wako ni upi?
Axact

Post A Comment: